Dullonet Job,Career and Latest Scholarship

Friday, October 30, 2009

JK azindua kituo cha yatima wilayani rungwe

JK akiwa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Lucy Hope Centre Bi.Lucy Mwandosya pamoja na Waziri wa Maji Profesa Mark Mwandosya muda mfupi baada ya kuwahutubia wananchi wa Lufilyo,Rungwe wakati wa uwekaji jiwe la Msingi katika jingo la taasisi hiyo uliofanyika jana.Taasisi ya lucy Hope inawahudumia watoto Yatima


JK akiwa na mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Lucy Hope Centre Bi.Lucy Mwandosya na Waziri wa Maji Profesa Mark Mwandosya wakishangalia wakati wa hafla ya kuweka jiwe la Msingi katika jingo la taasisi hiyo iliyofanyika huko Lufilyo,Rungwe, mkoani Mbeya jana jioni.Taasisi ya Lucy Hope inawahudumia watoto Yatima kwa kuwalea na kuwapa elikmu katika ngazi mbalimbali.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Lucy Hope Centre Bi.Lucy Mwandosya na Mumwewe Profesa Mark Mwandosya wakimkabidhi JK picha iliyochorwa na Bi.Lucy mwandosya inayoonesha ngoma ya utamaduni ya Rungwe ijulikanayo kama " Ndingala" wakati wa hafla ya kuweka jiwe la msingi katika jengo la taasisi hiyo huko Lufilyo Rungwe jana jioni.
Picha na Freddy Maro


Read more...

Wednesday, October 28, 2009

Mabadiliko ya tovuti

Naomba nafasi katika blogu yako kuwataarifu wasomaji kuwa tovuti ya mpya ya wavuti.com imechukua nafasi ya iliyokuwa nukta77.com na nukta77.blogspot.com

Naomba yeyote aliyekuwa ameweka linki ya nukta77 aihariri na kuweka wavuti.com

Karibuni sana kutembelea kwa taarifa za nafasi za masomo na kazi kwa burudani na bila kusahau habari na porojo!

Asanteni.

wavuti.com

Read more...

Monday, October 26, 2009

Dk. Salim Ahmed Salim aizungumzia Richmond


Dk. Salim Ahmed Salim akiongea na
wanahabari nyumbani kwake jijini Dar
MKUTANO WA DK. SALIM AHMED SALIM NA VYOMBO VYA HABARI
LEO JUMAPILI, TAREHE 25. 10. 2009585 MSASANI PENINSULA,
DAR ES SALAAM
Mabibi na Mabwana.
Habari za asubuhi
Nawashukuru nyote kwa kuja kwenu.
Mtakumbuka kuwa mapema mwaka huu, Bodi ya Taasisi ya Mo Ibrahim, ambayo mimi ni mjumbe mmoja wapo, ilitoa uamuzi wa kufanya sherehe za kutunuku Tuzo ya Mafanikio ya Uongozi Bora Barani Afrika, hapa Dar es Salaam.
Kutokana na uamuzi wa Kamati ya Tuzo ya Mo Ibrahim mapema mwezi huu wa kutomtunukia yeyote Tuzo hiyo, hapatakuwa na sherehe ya kutoa Tuzo kama ilivyopangwa hapo awali.
Hata hivyo, tumeamua kuitumia nafasi hii kutilia mkazo umuhimu wa Uongozi Bora barani Afrika. Kufuatia uamuzi huo, matukio muhimu mawili yameandaliwa.

Tukio la kwanza litakalofanyika jioni tarehe 14 Novemba, 2004 ni la kiutamaduni ambalo, licha ya shughuli nyinginezo, watakaohudhuria wataweza kushuhudia michango ya wasanii mahiri kama Yossou N’Dour na Angelique Kidjo, tukio ambalo litatangazwa moja kwa moja katika radio na runinga mbalimbali barani Afrika.
Sherehe hizo zitahudhuriwa na watu mashuhuri waliotoa mchango mkubwa kwa bara la Afrika pamoja na mamia ya watanzania na wageni mbali mbali kutoka pande zote za dunia.
Aidha, tukio hilo litatoa kipaumbele kuhusu nafasi, majukumu na wajibu wa vijana barani Afrika hivi sasa na katika siku za usoni.

Tukio la pili ambalo linazinduliwa kwa mara ya kwanza kabisa na Taasisi ya Mo Ibrahim, litakuwa ni Jukwaa (mbonge) ambalo litakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo Viongozi, Maofisa wakuu wa serikali, Wafanyabiashara, Wanaharakati, Wasomi, Wanafunzi na Vijana kutoka nchi mbali mbali barani Afrika, ili kujadiliana mada mbalimbali zinazohusu fursa na mambo muhimu ya maendeleo.
Jukwaa litafanyika siku ya Jumapili, tarehe 15 Novemba 2009.
Kimsingi, lengo la jukwaa hilo ni kujadili na kuweka bayana fikra na mtazamo wa pamoja wa jinsi ya kushughulikia masuala ya maendeleo kwa siku za usoni.Jukwaa hilo litakuwa na Mada kuu Tatu zitakazojadiliwa katika vipindi vifuatavyo:
Mjadala wa mada ya kwanza, utahusu Haki na Mabadiliko ya Hali ya Hewa Duniani (Climate Change and Climate Justice).
Mwenyekiti atakuwa Rais Mstaafu Festus Mogae wa Botswana.
Rais Mogae ni Mtunikiwa wa Tuzo ya Taasisi ya Mo Ibrahim kwa mwaka 2008, na ni miongoni mwa wawakilishi wanne maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki-moon, kuhusiana na masuala ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa.
Mjadala wa mada ya pili, utahusu Kilimo na Usalama wa Chakula (Agriculture and Food Security).
Mwenyekiti wa mjadala huo atakuwa Katibu Mkuu Mstaafu wa Umoja wa Mataifa, Bwana Kofi Annan.
Bw. Annan ni Mwenyikiti wa Bodi ya Mshikamano wa Mapinduzi ya Kijani katika Afrika – AGRA.
Mjadala wa mada ya tatu, utahusu Ushirikiano wa Kikanda wa Kiuchumi (Regional Economic Intergration) ambao Mwenyekiti wake ni Bwana Abdoulie Janneh.
Bwana Janneh ni Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Uchumi ya Afrika ya Umoja wa Mataifa.
Mkutano huu utakuwa ni Muhimu, utakaowaleta watu kutoka sehemu zote za Afrika.
Wadau wote hawa wanakuja pamoja wakati ambapo kwa upande mmoja kuna maendeleo ya jumla katika bara la Afrika lakini kwa upande mwingine kuna vikwazo vya kutia wasiwasi katika baadhi ya nchi na hivyo kujenga umuhimu wa wadau na taasisi mbalimbali kukutana na kutafuta ufumbuzi na changamoto ambazo zinakabiliwa barani la Afrika.

Kwa kufanya hivyo, tutaendeleza mjadala na mazungumzo kuhusu changamoto za msingi ambazo zinakabili bara la Afrika.
Taasisi ya Mo Ibrahim inaamini kuwa ili kutoa mchango madhubuti katika juhudi za kuendeleza uongozi bora katika Afrika, taasisi haina budi kusaidia kufanikisha mijadala na mazungumzo mbalimbali yanoyohusu changamoto za msingi za muda mrefu zinazolikabili bara letu.
Baada ya kueleza hayo, ninapenda kutoa ufafanuzi kuhusu kazi moja kubwa ya Taasisi ya Mo Ibrahim, kazi ambayo tunaiona kuwa muhimu zaidi kuliko Tuzo yenyewe.
Kazi hiyo ni ile kazi ambayo tathmini yake huwa ni mojawapo ya vigezo muhimu katika uamuzi wa kupatikana kwa TUZO.

Ninakusudia kueleza Vigezo vya Taasisi ya Mo Ibrahim kuhusu Uongozi Bora barani Afrika (Ibrahim Index on African Governance), chombo maridhawa katika juhudi za kuendeleza uongozi katika Afrika.
Tarehe 5 Oktoba mwaka huu tulitangaza vigezo hivyo huko Cape Town, Afrika ya Kusini.
Vigezo hivyo ni vipimo kamili vya kupimia usawa katika uongozi.

Ni kipimo cha uongozi bora ambacho hutoa taarifa na kuwawezesha wananchi kuendesha serikali na taasisi zao kwa kuwajibika.
Hivyo vigezo vilivyoandaliwa na Taasisi ya Mo Ibrahim ni pamoja na michango ya watafiti maarufu, taasisi, na ule mchango wa Kamati ya Ushauri ambayo inajumlisha Wasomi wa Afrika na Watafiti.
Vinalenga kuchachua mjadala kwa njia makini inayoweka misingi imara katika uongozi bora katika Afrika.
Vigezo vya Taasisi ya Mo Ibrahim hupima pia kwa kiasi gani huduma zinawafikia wananchi kupitia serikali na asasi zisizo za serikali.
Vigezo vya Mo Ibrahim vimezingatia misingi mikuu minne kama ifuatavyo:
1. Usalama na Utawala wa Sheria
2. Ushirikishaji na Haki za Binadamu
3. Fursai na Uchumi Endelevu
4. Maendeleo ya Watu

Tathmini ya Taasisi ya Mo Ibarahim hupima utawala bora kwa kutumia vigezo 84 ambavyo hukusanywa kwa hali ya kutosheleza inayohusisha taarifa na takwimu (data) ambazo zinatathmini uongozi bora barani Afrika.
Vigezo vinahusisha:
Usalama wa mtu BinafsiUtoaji wa Elimu na Ubora wa Elimu yenyeweHaki za Watu (Civil Liberties)Ubora wa MiundombinuUhuru wa MahakamaVigezo vimegawanywa tena katika sehemu ndogo ndogo (Sub-categories) kumi na tatu zikiwemo:
-Usalama wa mtu BinafsiUtawala wa SheriaHaki za Binadamu(Usawa) wa JinsiaMenejimenti ya UchumiMazingira na Maendeleo ya VijijiniElimuSasa ningependa kugusia suala la TUZO.
Kama mnavyojua, Kamati ya Tuzo haikuweza kuteua mshindi mwaka huu.

Kwa niaba ya Bodi ya Taasisi ya Mo Ibrahim, Rais mstaafu wa Botswana Ndugu Kitumire Masire alisoma tamko la Kamati ya Tuzo kama ifuatavyo:

“Taasisi ya Mo Ibrahim iko mstari wa mbele kusaidia uongozi wa Afrika ili kusukuma mbele hali ya Uchumi na Ustawi wa jamii wa watu wa Afrika.
Lengo la Taasisi ni kuendeleza na kuinua uongozi bora na kutambua umahiri katika uongozi wa Afrika.
Kamati ya Tuzo inatambua maendelea yaliyofikiwa katika baadhi ya nchi za Afrika kuhusiana na uongozi bora na wakati huo huo kuzingatia matatizo yaliyopo katika baadhi ya nchi.

Mwaka huu Kamati ya Tuzo iliwazingatia baadhi ya viongozi wenye sifa na kuheshimika (Credible) lakini baada ya kuzingatia kwa undani na umakini Kamati haikuweza kuchagua mshindi.”
Muundo wa Kamati ya Tuzo unajumlisha viongozi mashuhuri duniani ambao wanaamini kwa dhati kuisadia Afrika katika mapambano yake katika maeneo mbali mbali.
Kamati hiyo ipo chini ya mwenyekiti aliyepokea Tuzo ya Amani ya Nobel, Katibu Mkuu Mstaafu wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan.

Wajumbe wengine wa Kamati hiyo ya Tuzo ni pamoja na Marti Ahtisaari, Rais Mstaafu wa Finland ambaye pia ni Mtunukiwa wa Tuzo ya Nobel, Mohamed El Baradei, ambaye ni Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki na Mtunukiwa wa Tuzo ya Nobel; Mary Robinson, Rais Mstaafu wa Ireland na Kamishna Mkuu wa zamani wa Umoja wa Matifa wa Haki za Binadamu; Aicha Bah Diallo, Waziri wa Elimu Mstaafu wa Guinea na Mkurugenzi Mkuu Msaidizi Mstaafu wa UNESCO pamoja na Mama Graca Machel, Kiongozi mashuhuri wa harakati za Haki na misaada ya kibinadamu na Mtetezi mkubwa wa Haki za Maendeleo ya Watoto.Mimi kama mmoja wapo wa wajumbe wa kamati hiyo ya TUZO, ningependa kusisitiza tu kuhusu maamuzi hayo na kauli iliyotolewa.
Mtakapoanza kuuliza maswali ni vema niwajulisheni waziwazi kwamba sitajibu maswali yeyote yale kuhusu mwenendo wa majadiliano ya Kamati ya Tuzo.
Kifungu cha 11 cha hadidu za rejea kinasema:“Majadiliano na viambatisho vyovyote vya Kamati ya Tuzo ni SIRI KUU. Mjumbe yeyote wa kamati ya TUZO haruhusiwi kutoa siri ya mwelekeo wa mazungumzo au matokeo ya kutofaulu kwa mtu yeyote yule na wakati wowote ule.
”Hata hivyo, kama mjumbe wa Bodi ya Taasisi, ningependa nitoe maono machache:Kwanza kabisa, Wajumbe wa kamati ya Tuzo huzingatia itikadi ya Tuzo na hufanya kazi kwa mujibu wa kanuni na miongozo iliyowekwa.
Wanafanya hivyo kwa misingi ya uhuru, uaminifu na bila upendeleo.
Pili, katika kumchagua mshindi, Bodi hutegemea kwamba Kamati ya Tuzo itatia maanani mambo kadhaa yakiwemo: Utendaji wa nchi kama ulivyopimwa kwa kutumia Vigezo vya Taasisi ya Mo Ibrahim pamoja na chambuzi nyingine zinazoheshimika na kukubalika.

Viongozi wanaostahili ni watendaji wakuu wa nchi au Serikali waliostaafu, ambao wamepata madaraka kwa njia ya uchaguzi huru na halali na kustaafu katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita; baada ya kuitumikia nchi kwa mujibu wa Katiba kama ilivyoainishwa wakati alipochukua madaraka.

Kwa mujibu wa maelezo haya, kipindi kinachozungumziwa hapa ni kile cha mwaka 2006, 2007 na 2008

Read more...

vodacom yaibuka na cheka time

Mkuu wa Mkuu wa Kitengo cha Huduma mpya cha Vodacom, Boniphace Emmanuel, akiwa na Mkurugenzi wa Mahusiano Mwamvita Makamba na Mkuu wa Udhamini na Mawasiliano George Rwehumbiza

Mwamvita Makamba na Boniface Emmanuel
wakiwa na Meneja masoko wa Vodacom Elly Ngowi wakionesha mabango ya Cheka Time

Read more...

X Plastaz represent africa at BET Hip Hop awards 2009

X Plastaz with dj Threesixty in Rio de Janeiro, Brazil

Gsan in action at the BET cypher


Gsan posing with rapper Wale


Gsan posing with rapper/actor Mos Def


Gsan posing with dj Premier and rapper KRS One




America's annual 'gathering of giants' pays tribute to Tanzanian hip hop

Rapper Gsan of the group X Plastaz from Arusha, Tanzania, is representing Africa in this year's edition of the BET Hip Hop Awards, broadcast on October 27 on BET (Black Entertainment Television) in the USA. Meanwhile, X Plastaz' dj/producer Threesixty is heard all around the world through his production for major hip hop artist Redman (Def Jam).

The annual BET Hip Hop Awards are watched by millions of hip hop fans across the United States. Especially the part of the show in which Gsan participates, titled the BET Hip Hop Awards cypher, is highly anticipated as it's a true gathering of giants in rap music.

The cypher, in which the artists go back to the raw essence of hip hop, sees legendary dj/producer Premier team up with emcees such as Mos Def, Black Thought, Eminem and Joe Budden. The section in which BET pays tribute to the growing popularity of hip hop from East Africa by including Gsan sees the Arusha-born rapper team up with veteran rapper KRS One along with newcomers Wale and Nipsey Hussle.

The inclusion of X Plastaz in this year's BET Hip Hop Awards came about when BET contacted X Plastaz, after seeing their music video 'Nini dhambi kwa mwenye dhiki' on the Youtube website.

'Nini dhambi' which has drawn over 400.000 views is one of the most popular East African music videos on the web. Gsan flew out to Brooklyn, New York where the cypher was pre-recorded in an empty factory building.

His contribution was a rap in Swahili over an old school loop, cut up by dj Premier. While Swahili language hip hop was something new for the other artists, KRS One and Premier were full of love for the African input into this year's cypher.After recording the cypher, Gsan attended the Awards ceremony which took place in Atlanta on October 10, and which will finally be broadcast next tuesday, October 27.

Says Gsan in an interview with Emcee Africa presenter Lee Kasumba: "Well, the Cypher segment was recorded in New York before the actual award ceremony. For me, it was just amazing to be there with people like Eminem, KRS One, DJ Premier playing the beats, and being able to showcase what I had.
Many people were blown away with what I did and asked me why I rhymed in Swahili ‘cause they wanted to understand. I was just like ‘English is not my first language, I speak it, I love it but you will be able to mess me up if I rhyme in English’.

There were emcees from all over the world in one setting, and I was happy to represent for Africa. I wasn’t starstruck, just glad to showcase what I did and could do with my American counterparts. I mean, think of it, we really have the same names, just one word changes, African American and African, do you understand what that means?"

Also this week, X Plastaz dj Threesixty (real name: Bamba Nazar) is being hailed as a breath of fresh air in hip hop as his production for Def Jam-artist Redman was distributed across the internet.
The beat reminds of the energetic old school sound of the late 1970's and is a sureshot dancefloor filler.

The song, titled 'Coc Back', is the first single off Redman's long awaited new album titled 'Reggie Noble 9.5' which will be released in December.
The video for 'Coc Back' will be out this week.

Watch Gsan from X Plastaz in the BET Hip Hop Awards cypher on tuesday, October 27 at 8 pm (EDT) on BET. Outside of USA the cypher can be watched on Youtube from the day after the Awards show.

Official BET Hip Hop Awards website:
http://www.bet.com/specials/hiphopawards09
X Plastaz website: http://www.xplastaz.com/
Dj Threesixty website: http://www.bambanazar.com/
Also see this clip in which dj Premier announced the participants of this year's BET Hip Hop Awards cypher (mispronouncing Gsan as 'Anson')

Read more...

Friday, October 23, 2009

MAPOKEZI YA VODACOM MISS TANZANIA MIRIAM GERALD YAFANA JIJINI MWANZA

Vodacom Miss Tanzania Miriam Gerald,akimkabidhi mafuta ya kula mmoja wa watoto waishio katika mazingira magumu Laurance Malimi(kushoto) katika maeneo ya Bwiru jijini Mwanza mara baada ya kuwasili rasmi katika jijini humo akitokea Dares Salaam.


Mzee Yahaya Msabaha (81)(kushoto)akisalimiana na Vodacom Miss Tanzania Miriam Gerald (kulia)kwenye ofisi za Vodacom jijini Mwanza alipoenda kupatiwa huduma za M Pesa, mara baada ya mrembo huyo kuwasili kutoka Dares Salaam (katikati)Mkurugenzi Mkuu wa masoko wa kanda ya ziwa wa Vodacom Tanzania Steven Kingu.

Jinsi maandamano ya mapokezi ya Vodacom Miss Tanzania Miriam Gerald yalivyofana jiji Mwanza





Vodacom Miss Tanzania Miriam Gerald,akiwapungia mkono wananchi wa jiji la Mwanza walipompokea leo jijini humo, aliyesimama kushoto ni mmoja wa waandaji wa Vodacom Miss Mwanza Anita Zimbire. Miriam anatarajiwa kufanyiwa sherehe kubwa LEO jioni jijini Mwanza katika kumkaribisha rasmi ambapo mgeni wa heshima atakuwa mkuu wa Mkoa wa Mwanza Abbas Kandoro

Read more...

Mbio za baiskeli kwa wenye ulemavu zafana Mwanza

Mshindi wa kwanza wa mbio za baiskeli(Vodacom Mwanza cycle challenge)Helena Mwendesha mwenye namba 0978 kwa upande wa wanawake walemavu walioshiriki kilometa 10 akielekea kumaliza mbio hizo na kujipatia ushindi ambapo alitumia dakika 50 sekunde 44 akifuatiwa na mshindi wa pili Exvelina Exsaveli aliyetumia saa moja na dakika 3. Mashindano hayo yameandaliwa na Vodacom Tanzania.


Baadhi ya washiriki wa mbio za baiskeli(Vodacom Mwanza Cycle Challenge)wakianza rasmi hizo za baiskeli za kilometa 10 zilizoshirikisha wanawake walemavu na wanaume walemavu,mbio hizo zilianzia kiwanda cha vivywaji baridi cha Pepsi hadi Nyamongolo na kurudi pepsi.
Baadhi ya washiriki wa mbio za baiskeli(Vodacom Mwanza Cycle Challenge)wakijiandaa kuanza mbio hizo za kilometa 10 zilizoshirikisha wanawake walemavu na wanaume walemavu,mbio hizo zilianzia kiwanda cha vivywaji baridi cha Pepsi hadi Nyamongolo na kurudi pepsi.


Mshindi wa kwanza wa mbio za baiskeli(Vodacom Mwanza cycle challenge)Omary Matangajo mwenye namba 0975 kwa upande wa wanaume walemavu walioshiriki kilometa 10 akielekea kumaliza mbio hizo na kujipatia ushindi





Mshindi wa kwanza wa mbio za baiskeli(Vodacom Mwanza cycle challenge)Omary Matangajo mwenye namba 0975 kwa upande wa wanaume walemavu walioshiriki kilometa 10 akielekea kumaliza mbio hizo na kujipatia ushindi ambapo alitumia dakika 28 sekunde 59 ,Mashindano hayo yameandaliwa na Vodacom Tanzania.


Mshindi wa kwanza wa mbio za baiskeli(Vodacom Mwanza cycle challenge)Omary Matangajo mwenye namba 0975 kwa upande wa wanaume walemavu walioshiriki kilometa 10 leo akielekea kumaliza mbio hizo na kujipatia ushindi ambapo alitumia dakika 28 sekunde 59 ,Mashindano hayo yameandaliwa na Vodacom Tanzania.





Read more...

Thursday, October 22, 2009

Leon H. Sullivan Foundation dishes out 65m/- to Manyatta school in Arusha

The Chairman of Blue Jewel Company Emmanuel Wado and SAEDF Executive Officer Malcolm Pryor shaking hands with students of Manyatta Primary School in Arusha


Chairman of the Leon H. Sullivan Sumits Ambassador Carlton Masters addressing the audience at Manyatta Primary School in Manyatta Village in Arusha

Ambassador Carlton Masters shaking hands with students of Manyatta Primary School in Arusha.


Ambassador Carlton Masters presenting a dummy cheque for 65m/- to the Arumeru District Commissioner Mercy Sila (L) to help rehabilitate the Manyatta Primary School . First Right is Emmanuel Wado the Chairman of Blue Jewel Company, 2nd right is SAEDF Executive Officer Malcolm Pryor


Read more...

Dk. Buriani azindua simu ya vodacom itumiayo mionzi ya jua

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Rais Dk.Batilda Buriani, akikata utepe leo jijini Dar kuizindua simu aina ZTE S312 ambayo betri yake inatumia mionzi ya jua pamoja na umeme. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Dietof Mare. Vodacom ni kampuni ya kwanza kuileta na kuiagiza nchini simu hiyo itayonufaisha sana wadau wa vijijini na hata mjini luku ikiisha

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Rais Dk.Batilda Buriani akiwa ameshika Kipeperushi cha simu aina ya ZTE S312, wakati wa uzinduzi wa simu hiyo ambayo inatumia mionzi ya jua na umeme, kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Dietof Mare.Uzinduzi huo ulifanyika leo jijini Dar

Read more...

Mambo yaiva mbio za baiskeli Mwanza

Meneja Masoko wa Vinywaji vya baridi vya Pepsi Vis Rao Mwanza (katikati)akiongea na waandishi wa habari juu ya udhamini wao katika mashindano ya mbio za baiskeli (kushoto)Meneja Mauzo wa Vodacom Tanzania kanda ya ziwa Benedict Emmanuel,Meneja wa kampuni ya ulinzi ya Knight Support Sameer Virji(kulia)Mashindano haya ya mbio za baiskeli yatakayofanyika 23 na 24 mwezi huu yameandaliwa na Vodacom Tanzania wakishirikiana na CHABATA.


Meneja Minuso (Matukio na Promosheni) wa Vodacom Tanzania Rukia Mtingwa(kushoto)akifafanua jambo wakati wakitangaza njia (route)zitakazotumika katika mashindano ya mbio za baiskeli ,wa pili kutoka kushoto Mwenyekiti wa kamati ya ufundi CHABATA Godfrey Jax, Meneja Mauzo wa Vodacom Tanzania kanda ya ziwa Benedict Emmanuel, Meneja Masoko wa Vinywaji vya baridi vya Pepsi Vis Rao Mwanza.Mashindano haya yatakafanyika tarehe 23 na 24 yameandaliwa na Vodacom Tanzania wakishirikiana na CHABATA.

Read more...

WAFANYA BIASHARA KUTOKA UJERUMANI WAJIONEA FURSA ZA UWEKEZAJI NCHINI

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Wafanyabiashara na wawekezaji toka Ujerumani waliokuja kujionea fursa za uwekezaji na biashara nchini, wafanyabiashara hao walimtembelea Ofisini kwake jijini Dar es salaam Oktoba 20, 2009.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Read more...

Wednesday, October 21, 2009

Chikawe azindua cheti kipya cha kuzaliwa

Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe akikata utepe kuzindua cheti kipya cha kuzaliwa, jijini Dar leo. Anayeshuhudia ni Katibu Mkuu wa wa wizara hiyo, Oliver Mhaiki. Cheti hicho kimetengenezwa kwa utaalamu wa hali ya juu kudhibiti kanyaboya

Read more...

TAMASHA LA BIASHARA KUFANYIKA JIJINI DAR

Bw. Ali Nizam Meneja Mkuu wa Nizam Exhibitions Company akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo leo wakati alipotangaza Tamasha la Biashara ambalo linatarajiwa kufanyika kwenye Viwanja vya Mwalimu J.K.Nyerere barabara ya Kirwa kuanzia Oktoba 28 mpaka Novemba 10 litakaloshirikisha nchi 11 kutoka mashariki ya kati, Asia na Afrika Mashariki kushoto ni Dr. Ellen Otaru-Okoedion mratibu wa tamasha hilo.

Read more...

Mambo ya Sayansi

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kipera iliyoko katika wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro, wakifanya moja ya majaribio ya masomo ya sayansi wakati wa tamasha la shule za sekondari lilizofanyika Chuo Kikuu cha Mzumbe.Kulia ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.

Read more...

Rais Kikwete awaapisha Makatibu wakuu wapya Ikulu

Rais Kikwete akiwa na Makamu wa Rais Dk. Ali Mohamed Shein na Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda wakipozi na maafisa waandamizi aliowaapisha Ikulu jijini Dar leo ambao wako nyuma yao. Toka shoto ni Sethi Kamuhanda (Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo) Christopher Sayi (Katibu Mkuu, Wizara ya Maji na Umwagiliaji), David Kitundu Jairo kuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini, Jaji Frederick M. Werema (Mwanasheria Mkuu wa Serikali), Prosper Mbena (Katibu wa Rais), Mbarak M. Abdulwakil (Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi), George Masaju kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye kasimama nyuma kabisa. Nyuma Kulia ni Mh. Peniel Lyimo

Katibu wa Rais Mpya Bwana Prosper Mbena(kulia) akipongezana na katibu mkuu mpya wa wizara ya Nishati na Madini Bwana David Jairo(kushoto) muda mfupi baada ya hafla ya kuwaapisha iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi.Kabla ya uteuzi mpya Bwana Jairo alikuwa Katibu wa Rais

Katibu mkuu mpya Wizara ya Habari utamaduni na Michezo Bwana Sethi Kamuhanda akila kiapo mbele ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi katika hafla ambayo Rais aliwaapisha Makatibu wakuu wanne wapya pamoja na Mwanasheria mkuu na Naibu wake. (picha na freddy Maro)






Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitaniana na Bertha Jairo(7) binti wa Katibu Mkuu Mpya wa Wizara ya Madini na Nishati Bwana David Jairo wakati wa hafla ya kuwaapisha makatibu wakuu wapya wa wizara mbalimbali zilizofanyika ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi.Kabla ya uteuzi mpya Bwana Jairo alikuwa katibu wa Rais.

Read more...

Tuesday, October 20, 2009

Ujumbe wetu katika mkutano wa Mabunge duniani


Mh. Spika Samwel Sitta anahudhuria mkutano wa umoja wa mambunge duniani a.k.a International Parliamentary Union (IPU) , mjini Geneva uswisi ambapo ameongoza ujumbe wa wabunge wanne na waziri mmoja toka Tanzania ambao ni Mh. Kilonsti Mpologomyi, Mhe. Suzan Lyimo, Mhe. Dr. Mwita haji, na Mhe. Idris Mtulia pamoja na Waziri Mhe. Margareth Sitta.

Mh. Spika Samwel Sitta akisalimiana na baadhi ya wabunge toka bunge la uingereza ambao wengi wao wamemiss matukio waliyoyafaidi wakiwa Tanzania kwenye mkutano wa 55 wa CPA.

Katibu wa spika, Daniel Eliufoo, akimfafanulia jambo Mhe. Dr. Idris Mtulia katika mkutano huo. Mbele ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, mhe. Magreth Sitta, ambaye nae anahudhuria mkutano huo. Kwa nyuma ni mhe. Dr. Mwita Haji.


Read more...

Saturday, October 17, 2009

MAKAMU WA RAIS DK. SHEIN AAGANA NA MABALOZI

Makamu wa Rais Dk Ali Mohamed Shein akiagana na Balozi wa Algeria hapa nchini Bwana bwana Abdelmoun AAM Ahriz kufuatia kumaliza muda wake wa kuiwakilisha nchi yake hapa Tanzania walipokutana Ikulu jana. Sambamba na Balozi wa Algeria Dk Shein pia aliagana na Balozi wa Iran bwana Mohsin Movahhedi Ghomi.

Makamu wa Rais Dk Ali Mohamed Shein akiagana na Balozi wa Algeria hapa nchini Bwana Abdelmoun AAM Ahriz kufuatia kumaliza muda wake wa kuiwakilisha nchi yake hapa Tanzania walipokutana Ikulu jana. Sambamba na Balozi wa Algeria Dk Shein pia aliagana na Balozi wa Iran bwana Mohsin Movahhedi Ghomi.

Read more...

MAKAMU WA RAIS AKIMPA POLE MMOJA WA WAFANYAKAZI WA OFISI YAKE


Makamu wa Rais Dk Ali Moihamed Shein akimpa pole Emmanuel Loth, ambaye amelazwa katika Hospitali ya TMJ Dar Es Salaam kufuatia kufanyiwa upasuaji wa kidole tumbo. Emmanuel ni mfanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais Dar Es Salaam.Picha/Clarence Nanyaro.. VPO

Read more...

Watu wachukua chao Kipawa

Mkazi wa Kipawa , jijini Dar es Salaam,Coustansia Kasale akipokea hundi ya malipo kwa ajili ya nyumba ambazo zitabomolewa kupisha upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam.(Picha na Yusuf Badi).

Read more...

Fiesta yafunika Musoma


Umati wa watu uliofika kwenye tamsha la fiesta one love 2009 usiku wa kuamkia leo

Mkurugenzi wa Clouds Media Group/Prime Time Promotions Bw.Joseph Kusaga akimsikiliza Mstahiki meya wa Musoma Bw. Swahibu Mohamed Iddi alipozindua tamasha la fiesta 2009 lililokwenda sambamba na utambulisho wa frikwensi mpya za redio Clouds Fm mkoa wa Mara ambayo ni 98.6

Read more...

US Doctors For Africa CEO Meets President Kikwete at Dar es Salaam State House

President Jakaya Mrisho Kikwete welcomes the founder and Executive Chairman of the US Doctors for Africa Ted Alemahyu at State House Dar es Salaam yesterday afternoon(photo by Freddy Maro).

Read more...

Friday, October 16, 2009

Sia apewa chake na TTB


Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii (TTB) Peter Mwenguo kushoto akimkabidhi kompyuta yenye thamani ya shilingi 1.1 Balozi wa Utalii nchini (Miss Domestic Tourism) Sia Ndaskoi katika hafla iliyofanyika kwenye ofisi za bodi hiyo jengo la IPS jijini Dar leo, anayeshuhudia katikati ni Maria Mmari Mkurugenzi wa Utalii Wizara ya Maliasili na Utalii, Sia pia amekabidhiwa cheki yenye thamani ya shilingi 2.2.

Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii nchini Peter Mwenguo akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa mikutano wa bodi hiyo leo wakati alipomkabidhi zawadi zake balozi wa Utalii nchini Miss Domestic Tourism baada ya kunyakua taji hilo kwenye shindano la Vodacom Miss tanzania mwanzoni mwa mwezi huu ambapo mrembo Miriam Gerald kutoka Mwanza aliibuka mshindi, kulia ni Maria Mmari Mkurugenzi wa Utalii Wizara ya Maliasili na Utalii na kushoto ni Hashim Lundenga Mkurugenzi wa kamati ya Miss Tanzania.


Read more...

NMB wadumisha mila na utamaduni katika kula pamba


bosi wa biashara wa benki ya nmb akiwa na bosi wa masoko wa benki hiyo imani kajura wakijian daa kujichanganya na wana NMB wenzao katika mnuso maalumu hoteli ya white sands ambako mabosi wote ikiwa ni pamoja na mameneja wa matawi yote nchini pamoja na mameneja waandamizi wa makao makuu walijichimbia wiki nzima kupanga mikakati mipya ya kuboresha huduma zao. na leo kila mmoja alitoka kwa pamba za kiafrika

mabosi wakila pozi kwa pamba za aina tofauti

Read more...

  © Dullonet template by Dullonet.com 2009

Back to TOP