Dullonet Job,Career and Latest Scholarship

Monday, May 3, 2010

Spika afungua Mkutano wa wadau wa Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini.

Spika wa Bunge Mhe. Samuel Sitta, akifungua rasmi kongamano la mwaka la wadau wa kuzuia na kupambana na Rushwa lililoandaliwa na Taasisi ya Kuzui na Kupambana na Rushwa nchini (PCCB). Kongamano hilo limefanyika leo katika Ukumbi wa Blue pearl, Ubungo Plaza Dar e es salaam ambapo Spika alikuwa mgeni rasmi. Picha na Owen Mwandumbya wa Bunge.

Wajumbe mbalimbali waliohudhuria kwenye kongamano hilo wakimsikiliza Spika wa Bunge Mh. Samwel Sitta.



Mgeni rasmi katika kongamano la wadau wa Kuzui na Kupambana na Rushwa nchini , Spika wa Bunge Mhe. Samuel Sitta, ( katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa Kongamano hilo limefanyika leo katika Ukumbi wa Blue pearl, Ubungo Plaza Dar e es salaam.. Picha na Owen Mwandumbya wa Bunge

Read more...

Biashara Barabarani.


Kutokana na wajasiriamali wengi hapa nchini kukosa mbinu na maarifa ya kutafuta masoko ya nje ya bidhaa zao, wengi wao wamekuwa wakiuza bidhaa hizo kiholela kama inavyoonekana pichani wajasiriamali hawa katika mji mdogo wa Chalinze wakitafuta wanunuzi kwenye mabasi mwishoni mwa wiki.Picha na Fadhili Akida

Read more...

Maandalizi ya Taifa Cup, Morogoro wapigwa tafu.


Mwakilishi wa Kampuni ya Bia Mkoa wa Morogoro Haidhuru Ngakoka (kulia) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Said Mwambungu (kushoto) fedha taslimu shilingi Milioni 1,500,000/= katika hafla iliyofanyika kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo, kama mchango wa kampuni hiyo kwa timu ya Moro stars, kwa ajili ya michuano ya Kombe la Taifa Cup 2010.

Timu hiyo inatarajia kuondoka leo (kesho) kwenda Mkoa wa Tanga kwa ajili ya kuanza mechi yake ya kwanza dhidi ya timu ya Mkoa huo. Ili kuweza kufanikisha maandalizi ya timu hiyo kiasi cha shilingi milioni nane kinahitika, wadau wa soka Mkoani hapa wameombwa kuchangia ili kuweza kufanikisha ushindi wa timu hiyo. Picha na Father Kidevu

Read more...

MKUTANO WA INVESTIMENT CLIMATE SUMMIT WAANZA JIJINI DAR ES SALAAM.

Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Benjamin Wiliam Mkapa katikati akisalimiana na ris Mstaafu wa Botswana Festus Mogaye huku Ofisa Mtendaji mkuu wa ICF Issa Omary akisikiliza kabla ya uzinduzi rasmi wa mkutano unaoja uboreshaji wa mazingira ya uwekezaji katika Afrika.

Katibu Mkuu wa Jumuia ya Afrika Mashariki Juma Mwapachu kushoto akisalimiana na Jaji Mkuu wa Tanzania Agustino Ramadhan wakati walipokuwa wakitoka nje mara baada ya uzinduzi wa mkutano huo.


Balozi wa Rwanda nchini Tanzania mama Fatma Ndagiza akitaniana na Katibu Mkuu wa Jumuia ya Afrika Mashariki Juma Mwapachu mara baada ya ufunguzi wa mkutano wa uboreshaji wa mazingira ya uwekezaji katika nchi za Afrika ulioanza leo kwenye hoteli ya Dubble Three Hilton jijini Dar es salaam.



Ofisa Mtendaji Mkuu wa ICF Issa Omary akimuongoza Rais Mstaafu wa Botswana Festus Mogaye kuingia kwenye chumba cha mkutano wakati wa uzinduzi wa mkutano unaojadili uboreshaji wa mazingira ya uwekezaji katika nchi za Afrika




Ofisa Mtendaji Mkuu wa The Investiment Climate Facility For Africa (ICF) Bw. Issa Omary akizungumza na waandishi wa habari na kufafanua mambo mbalimbali yatakayozungumzwa katika mkutano wa uboreshaji wa mazingira ya uwekezaji katika nchi za Kiafrika hasa kwa wafanya biashara wadogo ambapo mkutano huo uliozinduliwa leo kwenye hoteli ya Dobble Three Hilton na utachukua siku mbili kabla ya ule wa World Economic Forum unaotarajiwa kufanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City hapa jijini Dar es salaam na kubudhuriwa na viongozi mbalimbali wa nchi za kiafrika na wataalam wa masuala ya uchumi.
Issa Omary amesema Kutatua matatizo ya uwekezajio katika Tanzania na nchi zingine za kiafrika na kuboresha wa huduma mbalimbali za kibiashara inawezekana tena kwa gharama ndogo sana kitu muhimu ni serikali husika kukaa na wadau mbalimbali na wafanyabiashara ili kupata msukumo wa pamoja katika kurekebisha kasoro mbalimbali zinazokabili huduma sekta mbalimbali za kibiashara
Ametolea mfano kuwa kwa nchi ya Rwanda ambayo kampuni zilikuwa zikisajiriwa kwa muda wa siku 30 lakini kwa sasa kampuni inasajiriwa kwa siku moja na gharama imeshuka kutoka dola 400 za kimarekani mpaka dola 45 jambo ambalo Rais Paul kagame mwenyewe alilisimamia na hatimaye wamefanikiwa.





Read more...

Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ali Sheni chapisho la (UN-HABITAT)

Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ali Sheni akifungua wa mkutano wa siku moja jana jijini Dar es salaam katika Ukumbi wa Karimjee wenye lengo la kujadili mikakati mbalimbali ya uimarishaji na uendelezaji wa wa Jiji la Dar es salaam jiji hilo.

Baadhi ya washiriki wa mkutano wa siku moja unaozungumzia uimarishaji na uendelezaji wa wa Jiji la Dar es salaam wakimsikiliza jana jijini humo Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ali Sheni wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.


Read more...

President Kikwete opens 2nd TICAD Ministerial meeting in Arusha.

President Jakaya Mrisho Kikwete and Japanese Minister for Foreign Affairs Katsuya Okada arrives at Arusha International Conference Centre for the opening ceremony of the 2nd TICAD Ministerial meeting yesterday morning(photos by Freddy Maro)

Minister for Foreign Affairs and International Cooperation Bernard Membe(centre) introduces to President Jakaya Kikwete Japan Minister for Foreign Affairs Katsuya Okada shorly after the President arrived at Arusha International Conference Centre(AICC) to open the second TICAD Ministerial Follow up meeting yesterday morning.















President Jakaya Kikwete delivers his opening speech during the 2nd TICAD Ministerial Follow meeting at AICC in Arusha yesterday morning.




Read more...

Hamis Hamad Mnondwa kumvaa Kigoda


Kijana Hamis Hamad Mnondwa akizungumza na waandishi wa habari kuelezea juu ya nia yake ya kumvaa mbuge Abdallah Kigoda wa Handeni ili kuchukua jimbo na kuanza kuwatumikia wananchi wa jimbo hilo.

Amesema wananchi wa Handeni hawahitaji kutawaliwa ila wanahitaji kuongozwa kwa kushauriana katika kuleta maendeleo ya jimbo hilo ambao liko nyuma sana kiuchumi, kielimu na kiafya pia, ameongeza kuwa yuko tayari kwa kuwatumikia wananchi wa Handeni kinachotakiwa ni wao kumuidhinisha ili aweze kuwatumikia.

Amesema utaratibu uliotangaza na chama cha mapinduzi unasema fomu zitaanza kutolewa kwa wagombea tarehe 26 mwezi julai na kurudishwa tarehe 28 mwezi huohuo, Hamis Hamad Mnondwa aliongozana na baba yake mzazi katika mkutano huo anayejulikana kwa jina la Njama Issa Mnondwa aliyeko kulia.

Read more...

Friday, April 16, 2010

WIZARA YA HABARI UTAMADUNI NA MICHEZO YAWAPIGA MSASA WAFANYAKAZI WAPYA


Baadhi ya washiriki wa mafunzo elekezi kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni na Michezo Bw. Seith Kamuhanda(hayupo pichani) wakati wa ufunguaji mafunzo elekezi leo mjini Dar es salaam.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni na Michezo Bw. Seith Kamuhanda akifungua mafunzo elekezi ya waajiriwa wapya wa Wizara hiyo leo mjini Dar es salaam. Mafunzo hayo ni sehemu ya utaratibu wa Serikali wa kuwaelimisha watumishi wake wapya kwa ajili ya kuongeza ufanisi mahali pa kazi.Picha na tiganya vincent-maelezo

Read more...

Bungeni Dodoma


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Mbunge wa Muhambwe, Felix Kijiko wakitoka kwenye ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma, Aprili 19, 2010.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akijadili jambo na Spika wa Bunge Samuel Sitta (kulia) wakati alipoongoza kikao cha wabunge hao kwenye ukumbi wa Msekwa, Bungeni Mjini Dodoma Aprili 18, 2010. Kushoto ni Kaimu Katibu wa wabunge wa CCM na Mbunge wa Peramiho, Jenista Mhagama. .(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Read more...

Ziara ya Wanasheria wa Tume Mbinga, Songea


Ofisa Sheria wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT) Flaviana Charles akionesha msisitizo wakati akiwasilisha mada ya Sheria ya Mirathi mbele ya Makatibu Tarafa na Wazee wa Mbinga mkoani Ruvuma.

Baadhi ya Makatibu Tarafa na Wazee wa Wilayani Mbinga mkoani Ruvuma wakifuatialia mada zilizokuwa zikitolewa na timu ya wanasheria wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania.


Baadhi ya Watumishi wa Serikali kutoka idara mbalimbali za Serikali Wilayani Mbinga mkoani Ruvuma wakifuatialia mada zilizokuwa zikitolewa na timu ya wanasheria wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania.


Ofisa Sheria wa Tume ya Kurekebisha Sheria (LRCT) Flora Tenga aliyesimama akizungumza mbele ya Watumishi wa Serikali kutoka idara mbalimbali wilayani Mbinga mkoani Ruvuma wakati timu ya wanasheria wa Tume ilipofanya ziara ya kutoa elimu ya sheria kwa umma wilayani humo, wengine ni Mwandishi Mkuu wa Sheria wa Tume Caritas Mushi katikati na Ofisa Sheria Flaviana Charles.

Read more...

Wanachama wapya wa UWT kutoka vyuo vya Dodoma wapewa kadi.

Naibu Kaibu Mkuu wa UWT Taifa Asha Bakari akimkabidhi kadi ya uanachama wa CCM Bi Situmai Makae wakati akiwaapisha wanachama wapya Wa UWT zaidi ya 800 jana mkoani Dodoma kutoka Vyuo vinne , CBE, Mipango, St Johns na UDOM.



Mpiga zeze maarufu nchini Dr. Masalia akipiga zeze katika sherehe hiyo juzi
Wanachama wapya wa UWT kutoka vyuo mbalimbali Mkoani Dodoma wakiapa kuwa watiifu kwa chama chao.Picha zote na Mwanakombo Jumaa.

Read more...

Mkulo na Mkukuta yake.


Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo(katikati) akibadilishana mawazo jana nje ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma na Mbunge wa Jimbo la Busega wilayani Magu, Mkoani Mwanza, Dk. Raphael Masunga Chegeni(kushoto) pamoja na Mbunge wa Viti Maalum CHADEMA Lucy Owenya ( kulia) mara baada ya kumalizika kwa kukusanya maoni ya wabunge juu mchakato wa majadiliano ya Mpango wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini Tanzania(MKUKUTA) ambazo zoezi hilo limeanza jana jioni na linaendelea nchini kote.


Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo(kulia) akibadilishana mawazo jana nje ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi Ramadhan Khijjah (katikati) pamoja na Naibu Katibu Mtendaji Ofisi ya Rais Tume ya Mipango Clifford Tandari( kushoto) mara baada ya uzinduzi wa mchakato wa majadiliano ya Mpango wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini Tanzania(MKUKUTA) ambazo zoezi hilo limeanza jana jioni na linaendelea nchini kote.

Read more...

President Jakaya Kikwete meets the UN Secreary General Ban Ki Moon at the UN Headquarters in New York

The UN Secretary General Ban-ki Moon welcomes President Jakaya Mrisho Kikwete at his UN Headquarters office in New York today for official talks



President Jakaya Mrisho Kikwete and the UN Secretary General Ban ki Moon withe their teams get down to business at the UN Heaquarters in New York today.Photos by Freddy Maro

Read more...

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AKUTANA NA MABALOZI WA AFRIKA KUSINI NA MALAWI

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Afrika ya Kusini, Radhia Msuya (katikati) na Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Patrick Tsere , Ofisini kwake Bungeni Mjini Dodoma, Aprili 16, 2010.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Afrika ya Kusini, Radhia Msuya (katikati)na Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Patrick Tsere , Ofisini kwake Bungeni Mjini Dodoma.


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Tekinolojia, Profesa Peter Msolwa wakitoka kwene ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma, leo Aprili 16, 2010. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Read more...

Serengeti yaibuka na promosheni mpya kwa wateja wake

Meneja Matukio na promosheni wa kampuni ya bia ya Serengeti(SBL) Bwana Bahati Singh, akionyesha kipeperesushi kinachoonesha zawadi mbalimbali kwa waandishi wa habari leo Dar es salaam. Kesho zawadi hizi zitatolewa kwenye viwanja vya Kinondoni Boafra and Mwembe yanga Temeke. Kulia ni na Afisa Habari Mwandamizi wa SBL Bwana Imani Lwinga



Meneja Matukio na promosheni wa kampuni ya bia ya Serengeti(SBL) Bwana Bahati Singh, akiongea na waandishi wa habari leo Dar es salaam akielezea kuhusu promosheni ya vuna pesa na Mizawadi Kede-kede itakayotolewa na SBL ambayo itaanza kesho katika viwanja mbalimbali jijini. Kesho zawadi hizi zitatolewa kwenye viwanja vya Kinondoni Biafra and Mwembe yanga Temeke. Kulia ni na Afisa Habari Mwandamizi wa SBL Bwana Imani Lwinga.

Read more...

MISS UNIVERSE WAINGIA KAMBINI KUJIWINDA NA KINYANG'ANYIRO APRILI 23.

Miss Universe wa mwaka 2009 Illuminata James, akimkagua mmoja wa waremmbo, Warembo wanaoshiriki mashindano ya Miss Universe 2010 , Nezia Anthony wakati wa kuanza rasmi kwa kambi yao katika Hoteli ya Giraffe Dar es salaam leo.




Mkurugenzi wa Kampuni yaCompas Communicatins Maria Sarungi ambaye pia ndiye mwandaaji wa Miss Universe Tanzania akiongea mbele ya wageni mbalimbali na warembo wakati warembo wapatao 20 walipoingia rasmi kambini kwa muda wa wiki moja katika hoteli ya Girrafe Ocean View Mbezi kujiandaa na shindano hilo linalotarajiwa kufanyika aprili 23 kwenye ukumbi wa Mlimani City baadae mwaka huu jijini Dar es salaam.
(picha na Mohamed Mambo)


Warembo wanaoshiriki mashindano ya Miss Universe wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa kuanza rasmi kwa kambi yao katika Hoteli ya Giraffe Dar es salaam leo.

Read more...

Thursday, April 15, 2010

AICC YASAINI MKATABA WA KUUNDA BARAZA LA WAFANYAKAZI

Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Elishilia Kaaya (kulia) akibadilishana na Katibu wa TUICO Mkoa wa Arusha, Hussein Ngowo mkataba wa kuunda Baraza la Wafanyakazi tawi la Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC). Mkataba huo ulisainiwa katika ofisi za AICC mjini Arusha. Kushoto ni Katibu wa TUICO tawi la AICC, Rashid H. Rashid.


Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Elishilia Kaaya (katikati) akibadilishana na Mwenyekiti wa TUICO tawi la Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Ezekiel Kiologwe mkataba wa kuunda Baraza la Wafanyakazi tawi la AICC. Mkataba huo ulisainiwa wiki hii katika ofisi za AICC, mjini Arusha. Kushoto ni Katibu wa TUICO Mkoa wa Arusha, Hussein Ngowo.


Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Elishilia Kaaya (katikati) akitia saini mkataba wa kuunda Baraza la Wafanyakazi tawi la AICC. Mkataba huo ulisainiwa wiki hii katika ofisi za AICC. Kushoto ni Katibu wa TUICO Mkoa wa Arusha, Hussein Ngowo na kulia ni Mwenyekiti wa TUICO tawi la AICC, Ezekiel Kiologwe na kulia kabisa ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa AICC, Savo Mung’ong’o. (Picha kwa hisani ya AICC) .

Read more...

Waziri Mkulo azindua mchakato wa maoni ya MKUKUTA awamu ya 2 mjini Dodoma


Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo (katikati) akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari juu ya kuanza kwa mchakato wa kujadili kuhusu Mpango wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini Tanzania (MKUKUTA) awamu ya pili. Mchakato wa kutoa maoni umeanza jana mjini Dodoma ambapo wabunge walipata fursa ya kutoa maoni yao jinsi ya kuboresha awamu ya pili ya MKUKUTA. wengine katika picha ni Naibu Katibu Mkuu wizara ya fedha na Uchumi John Haule (kushoto) na Mkurugenzi wa Idara ya Kuondoa Umaskini na Uwezeshaji Anna Mwasha(kulia)

Read more...

Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge yatembelea VOA


Matembezi ya kamati ya mambo ya nje ya bunge ikiwa katika ofisi za VOA, Kutoka kushoto Khadija Riyami,Wilson Masilingi,Juma Nkamia 'Kocha Mtangazaji' , Afisa Ubalozi Suleiman Saleh,Mh.Juma Killimba,Mkamiti Kibayasi na Mariam Kurtz.

Read more...

Bungeni Dodoma

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma, Aprili 15, 2010


Baadhi ya Makatibu Wakuu, Naibu Makatibu Wakuu na Makatibu Tawala wa Mikoa wakimsikili Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati alipofungua mkutano wao kwenye ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha ST. Gaspar Conference Cetre Mjini Dodoma leo.


Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo akifungua mkutano wa Makatibu Wakuu, Naibu Makatibu Wakuu na Makatibu Tawala wa Mikoa wanawake kwenye ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha ST. Gaspar Conference Cetre Mjini Dodoma

Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo (waliokaa watano kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Makatibu Wakuu, Naibu Makatibu Wakuu na Makatibu Tawala wa Mikoa baada ya kufungua mkutano wao wa mwaka kwenye ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha ST. Gaspar Conference Cetre Mjini Dodoma,





Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akijibu maswali ya wabunge, bungeni mjini Dodoma, Aprili 15,2010.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Ta, Dr. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akifurahia jambo katika Mazungumzo na Mbunge wa Peramiho, Jenista Mhagama kwenye viwanja vya Bunge Aprili 15, 2010.




Read more...

  © Dullonet template by Dullonet.com 2009

Back to TOP