Dullonet Job,Career and Latest Scholarship

Monday, May 3, 2010

Maandalizi ya Taifa Cup, Morogoro wapigwa tafu.


Mwakilishi wa Kampuni ya Bia Mkoa wa Morogoro Haidhuru Ngakoka (kulia) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Said Mwambungu (kushoto) fedha taslimu shilingi Milioni 1,500,000/= katika hafla iliyofanyika kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo, kama mchango wa kampuni hiyo kwa timu ya Moro stars, kwa ajili ya michuano ya Kombe la Taifa Cup 2010.

Timu hiyo inatarajia kuondoka leo (kesho) kwenda Mkoa wa Tanga kwa ajili ya kuanza mechi yake ya kwanza dhidi ya timu ya Mkoa huo. Ili kuweza kufanikisha maandalizi ya timu hiyo kiasi cha shilingi milioni nane kinahitika, wadau wa soka Mkoani hapa wameombwa kuchangia ili kuweza kufanikisha ushindi wa timu hiyo. Picha na Father Kidevu

0 comments:

Post a Comment

  © Dullonet template by Dullonet.com 2009

Back to TOP