Dullonet Job,Career and Latest Scholarship

Tuesday, October 13, 2009

JK ndani ya Musoma

JK akiteta jambo na Meneja wa TANESCO kanda ya Ziwa Bwana Makala Kingu muda mfupi baada ya kuzindua mradi wa umeme katika kijiji cha Kisamwene, kata ya Butuguri wilaya ya Musoma vijijini jana jioni


JK akibonyeza kitufe wakati akizindua mradi wa umeme katika kijiji cha Kisamwene kata ya Butuguri,wilaya ya Musoma vijijijni jana jioni

JK akiongea na mwanafunzi Ezekiel James wakati alipokagua darasa la mfano muda mfupi baada ya kufungua shule ya Sekondari ya Chifu Oswald Mang’ombe jana jioni wilaya ya Musoma vijijini.



Mwanafunzi Godbless Buluhya wa shule mpya ya sekondari ya Chifu Oswald Man’gombe iliyopo musoma vijijini akifanya jaribio la kisayansi wakati JK alipokagua maabara ya shule hiyo jana jioni.Wengine katika kutoka kushoto ni Mama Salma Kikwete, Mkuu wa Mkoa wa Mara Kanali Mstaafu Enos Mfuru(wapili kushoto) na wanne kulia ni Mbunge wa Musoma vijijini Mh. Nimrod Mkono.

JK akimpongeza mbunge wa Musoma vijijini Nimrod Mkono kwa kujenga shule ya kisasa ya mchepuo wa Sayansi ya chifu Oswald Mang’ombe na hatimaye kuikabidhi kwa serikali katika hafla fupi iliyofanyika shuleni hapo jana jioni.Mheshimiwa Mkono aliijenga shule hiyo kwa kutumia mapato yake mwenyewe akisaidiwa na marafiki na wafadhili mbalimbali.




JK akifunua kitambaa kuzindua rasmi Shule ya sekondari mchepuo wa Sayansi ya Chifu Oswald Mang’ombe iliyopo wilaya ya Musoma vijijini.Pembeni ni Mbunge wa Musoma vijijini Mheshimiwa Nimrod Mkono ambaye ndiye mfadhili mkuu wa shule hiyo






Mama Maria Nyerere akimkaribisha JK muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Musoma jana jioni. JK yupo mkoani Mara kukagua na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo ambapo pamoja na shughuli nyingine atakuwa mgeni rasmi katika kilele cha mbio za mwenge siku ya Jumatano ambayo pia itakuwa ni kuadhimisha siku ya Nyerere.





0 comments:

Post a Comment

  © Dullonet template by Dullonet.com 2009

Back to TOP