Dullonet Job,Career and Latest Scholarship

Monday, October 5, 2009

Mashindano ya uvuvi ya Vodacom yafana

Mkuu wa Yacht Club Comodere Spiros (kushoto) akimkabidhi kikombe cha ushinda wa uvuvi wa kutumia boti Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Dietlof Mare baada ya kuibuka mshindi katika mashindano hayo yaliyofanyika katika Kisiwa cha Sinda katika Bahari ya Hindi jumla ya nchi Nne zilishiriki Mashindano hayo,mwishoni mwa wiki.


Mkuu wa udhamini na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania George Rwehumbiza(kushoto)akiwa katika picha ya pamoja na wenzake waliposhiriki katika mashindano ya kuvua samaki


Watoto wakiwashangaa samaki waliovuliwa jinsi walivyokuwa wakubwa.
Washindi wa shindano la kuvua samaki kwa kutumia maboti wa Timu ya Black Widow wakiwa katika,picha ya pamoja baada ya kuibuka washindi (kushoto) Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Dietlof Mare, Linda Wiechers Raoul Dippenaar,na Christo Human wakiwa na vikombe vyao katika kisiwa cha Sinda kilichopo katika Bahari ya Hindi,Mwishoni mwa wiki.





Samaki mkubwa aina ya Papa mwenye kilo 157 aliyekuwa mkubwa zaidi baada ya kuvuliwa na Len Botha wa Afrika Kusini katika shindano la Maboti ya kuvua samaki akipimwa kwenye muzani katika kisiwa cha Sinda, shindano hilo lilizishirikisha Nchi Nne yakiwa yamedhaminiwa na Vodacom Tanzania,Mwishoni mwa wiki.


0 comments:

Post a Comment

  © Dullonet template by Dullonet.com 2009

Back to TOP