Dullonet Job,Career and Latest Scholarship

Saturday, August 22, 2009

michango ya vodacom marathon yawafikiwa walengwa


Meneja mauzo wa Vodacom Tanzania kanda ya Dares Salaam Atilio Lupala akiwakabidhi watoto yatima wa kituo cha mbagala chamanzi moja msaada wa ndoo ya mafuta ya kula yenye thamani ya shilingi milioni 6 yaliyotokana na ukusanyaji wa fedha katka mbio za Vodacom Dar Marathoni,yaliyodhaminiwa na KCB benki,Pepsi,Ultimate Security,Clouds Fm.


Kutoka kushoto Meneja Matukio na Promosheni wa Vodacom Rukia Mtingwa, Meneja Masoko wa Ultimate Security Moses Omuteku na Meneja wa huduma kwa wateja Benki ya KCB Thereza Majinge(kulia)wakikabidhi msaada wa vyakula vilivyotoka na malipo ya fomu za Vodacom Dar Marathoni vyenye thamani ya shilingi milioni 6 kwa kaimu katibu mkuu wa kituo cha kulea watoto yatima cha Mbagala Chamanzi.


Meneja mauzo wa Vodacom Tanzania kanda ya Dares Salaam Atilio Lupala akimkabidhi msaada wa moja ya vifaa vya Michezo vyenye thamani ya shilingi milioni 6 pamoja na vyakuala Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha Dares Salaam Captain Mstaafu Lucas Nkungu(kulia) kwa ajili ya kuendeleza Mchezo wa riadha kwa vijana.Vyote hivyo vilipatikana kutokana na ukusanyaji wa fedha katika mbio za Vodacom Dar marathoni. Hafla hii ilifanyika katika kituo cha kulelea watoto yatima cha Mbagala Chamanzi.

0 comments:

Post a Comment

  © Dullonet template by Dullonet.com 2009

Back to TOP