Dullonet Job,Career and Latest Scholarship

Saturday, August 15, 2009

Ras Makunja na vitu vyake

Mwanamziki wa Tanzania Ebrahim makunja aka Ras Ebby Makunja maarufu pia kama "Bw.Kichwa Ngumu" anayeiongaza bendi maarufu ya muziki wa dansi barani Ulaya "The Ngoma Africa" aka FFU, inasemekana ndiye mwanamziki wa mwanzo mmatunbi kutinga katika jarida la masupastaa na macelebrity la ujerumani, Star View magazine (Stern) yaani nyota,kuwemo katika jarida hilo inamaana unakubalika na katika kila hali kuwa moto wake kiusanii ni mkali !

Huyu bwana hapa katika picha www.view.stern.de/fc/picture/687997 huwa wanaandikwa katika majarida makubwa ya Ughaibuni watu ambao ni maarufu sana barani ulaya , hiyvo inaonyesha kuwa Ras Makunja ni kamanda anayeongoza na kumiliki kikosi hatari "The Ngoma Africa" kinachowadatisha akili mashabiki wengi kwa ya dansi lao,Ras Makunja anatarajiwa kutingisha jukwaa la Afrika Festival Hamburg City.

Ujerumani,siku ya Ijumaa ya 21-08-2009 ,oyesho hilo la wazi litafanyika katikati ya jiji la Hamburg-Altona,ambako mwaka jana walifanikiwa kuwatingisha mashabiki zaidi ya 50,0000 na kuwapa kazi ngumu walinzi katika onyesho hiliwasikilize http://www.myspace.com/thengomaafrica pia wanapatikana hapa http://www.facebook.com/ngomaafrica

0 comments:

Post a Comment

  © Dullonet template by Dullonet.com 2009

Back to TOP