Dullonet Job,Career and Latest Scholarship

Wednesday, March 31, 2010

Wawili wapiga hodi kwa Ndesamburo


Bwana Batista Mwendivita ambaye ni Mjumbe wa halmashari kuu ya Wilaya ya Moshi Mjini CCM na Mwenyekiti wa chama cha wenye ulemavu mkoani Kilimanjaro kushoto na MwanaCCM mwingine Gibson Nderangusho wakitangaza mbele ya wanahabari kwa pamoja nia yao ya kugombea ubunge katika jimbo la Moshi Mjini kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi CCM, wote kwa pamoja wamesema wana nia hiyo na katiba zote mbili ya Chama Cha Mapinduzi na ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania zinawaruhusu kufanya hivyo na ni haki yao ya kimsingi , marafiki hao wawili walitangaza nia yao leo kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo.

0 comments:

Post a Comment

  © Dullonet template by Dullonet.com 2009

Back to TOP