Iringa wamuaga Hajat Amina Mrisho Said
Aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Iringa ambaye kwa sasa mkuu wa mkoa wa Pwani Hajat Amina Mrisho Said (kushoto) akiwa amekabidhiwa ngao ya ushindi wa mapambano dhidi ya Rushwa ndani ya mkoa wa Iringa iliyotolewa na chama cha makandarasi mkoa wa Iringa,mkuu huyo anaagwa usiku huu katika ukumbi wa Ruco ambako sherehe zinaendelea ikiwa ni pamoja na kumkaribisha mkuu mpya wa mkoa wa Iringa Mohamed Abdulaziz na katibu tawala wake Bibi Getrude Mpaka maarufu kama mama Mchapa anayechoka bila kupumzika.
Mkuu wa mkoa wa Iringa Bw Mohamed Abdulaziz akiwa na aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Iringa Bibi.Amina Mrisho Saidi ambaye amehamishiwa mkoa wa Pwani ,Amina amepongezwa na kila mdau wa maendeleo mkoa wa Iringa na kupewa baraka zote katika kinyang'anyiro cha ubunge jimbo la Kiteto kuwa wana Kiteto wamempata mwanachama mchapa kazi wasema viongozi wa CCM mkoa wa Iringa. Picha zote na Francis Godwin wa Iringa
0 comments:
Post a Comment